PARIS, Ufaransa
KIUNGO wa Ufaransa, Samir Nasri ameomba radhi waandishi wa habari
kutokana na matamshi yake aliyoyatoa baada ya timu yake kutolewa katika
Fainali za Euro 2012 kwa kufungwa na Hispania.
Nasri alishambuliwa na vyombo vya habari baada ya kuwatolea kauli
chafu hasa baada ya timu yake kutolewa na Hispania kwa mabao 2-0.
"Naamini mashabiki na watu wengine walishangazwa na matamshi yangu,
lakini yote ni hasira za kufungwa, naomba radhi," Nasri aliandika kwenye
ukurasa wake wa twitter.
"Naipenda Ufaransa, soka na pia nawapenda mashabiki wote."
Nasri, anayeichezea Manchester City, hakuwaomba radhi mashabiki mara
baada ya matamshi yake: "Naweza kusema ni suala binafsi kati yangu na
waandishi wa habari. Nitazungumza zaidi siku itakapowadia."
Kocha wa Ufaransa, Laurent Blanc alisema tabia ya Nasri haikumfurahisha yeye pamoja na wachezaji wengine.
"Lilikuwa tatizo kweli kati ya Samir na waandishi wa habari," Blanc aliiambia televisheni ya Ufaransa.
|
No comments:
Post a Comment