MSHAMBULIAJI wa Azam FC, John Bocco, jana Alhamisi alitarajiwa
kumaliza rasmi majaribio ya wiki mbili ya kuwania kusajiliwa na klabu ya
SuperSport United ya Afrika Kusini.
Bocco ambaye alionyesha kiwango kizuri kwenye michuano ya Kombe la
Kagame mwezi uliopita, aliitwa na klabu hiyo kwa ajili ya majaribio na
kutimka Agosti 11, mwaka huu.
Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd
alisema mpaka sasa bado wanasubiri majibu kutoka katika klabu hiyo
inayoshiriki ligi kuu nchini humo.
Alisema nafasi hiyo ilianza
kugombewa na wachezaji tisa, wakachujwa wakabaki wanne akiwemo Bocco,
ambapo amesema kuwa anayetakiwa ni mmoja. “Bado tunasubiri majibu,
nafikiri akisharudi ndiyo tutajua, |
No comments:
Post a Comment