![]() |
| Marek Hamsik, Vladimir Weiss, Karim Guede
na Miroslav Stoch hawatolipwa posho zao zamichezo yote ya kufuzu kombe
la dunia watakayoichezea timu yao ya Taifa ya Slovakia kwa sababu
wachezaji hao walienda disko baada ya mechi ya Ijumaa dhidi ya
Lithuania. Ingawa usiku walioenda disko ulikuwa baada ya mechi,
wachezaji hao bado walikuwa kwenye kambi ya timu ya taifa na
ikizingatiwa Slovakia walikuwa na mchezo mwingine wa kufuzu dhidi ya
Liechtenstein siku nne zilizofuatia (Slovakia walishinda 2-0) Kutoka Football Italia: Wachezaji wawili wa Seria A pamoja nana mchezaji wa Freiburg Karim Guede na wa Fenerbache Miroslav Stoch, waliripotiwa kwamba walitoka usiku mjini Vilnius baada ya mchezo wao wa sare ya 1-1 dhidi ya Lithuania wiki iliyopita. Kwa mujibu wa La Republic, chama cha soka cha Slovakia waliamua kuwapa adhabu ya kutolipwa posho katika mechi zote zilizobaki za kufuzu wachezaji wote waliotoka na kwenda disko.Kwa kawaida ya Slovakia kwa kosa kama walilofanya akina Merek - mchezaji au wachezaji huwa wanapewa adhabu ya kusimamishwa. Lakini kwanini haikuwa hivyo kwa wachezaji hao. Mmoja wa watu wa ndani wa shirikisho wanalsema - walitaka kuendelea kufanya vizuri na kupata matokeo - wachzaji watatu kati ya wanne waliopewa adhabu walianza dhidi ya Liechtenstein. |
PSI
Saturday, September 15, 2012
MEREK HAMSIK NA WENZAKE KUTOLIPWA POSHO ZOTE ZA TIMU YA TAIFA KWA KOSA LA KWENDA DISKO WAKIWA KAMBINI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment