PSI

PSI

Thursday, November 22, 2012

OMBI LA DROGBA KUJIUNGA KWA MKOPO NA KLABU NYINGINE LAKATALIWA NA FIFA

Ombi la uhamisho wa usajili wa mkopo nje ya dirisha la
  usajili la Didier Drogba limekataliwa na FIFA.
Gwiji huyo wa zamani wa The Blues amekuwa akihusishwa
  na kurudi Chelsea kwa uhamisho wa mkopo wa muda
mfupi wakati wa mapumziko ya ligi kuu ya China lakini
FIFA leo wamekataa maombi ya nahodha huyo wa Ivory Coast.
Shirikisho hilo la soka duniani lilisema kwenye taarifa
  yake: "Tunathibitisha kwamba tulipokea maombi ya
mchezaji Didier Drogba kuomba ruhusa ya kusajiliwa nje
 ya kipindi cha usajili kwa mkopo.
"FIFA imemualifu mchezaji juu ya kanuni
zilizopo.....kwamba wachezaji wanaweza kusajiliwa katika
vipindi viwili tu vya mwaka vya usajili vilivyowekwa na
vyama vya soka."
FIFA ilisema ingewezekana tu kwa Drogba kuhama kama
asingekuwa na mkataba na kalbu nyingine ndio angeweza
kusajiliwa kwa wakati ulio nje ya dirisha la usajili.
Drogba alikuwa anahitaji kupata sehemu ya kuendelea
kujifua kabla ya kwenda kwenye michuano ya mataifa huru
ya Afrika 2013.


No comments: