PSI

PSI

Friday, April 26, 2013

WESTHAM NA MAN CITY KESHO KUHUSU MAREHEMU MARC VIVIEN FOE


Mashabiki wa timu za West Ham United na Manchester City kwa kushirikiana na uongozi wa timu zote mbili watafanya ishara ya kumkumbuka mchezaji wa zamani aliyewahi kuzichezea klabu zote mbili na timu ya taifa ya Cameroon Marehemu Marc Vivien Foe .
Mchezaji huyo aliyefariki dunia uwanjani wakati akiichezea timu yake ya taifa katika mchezo dhidi ya Colombia kwenye michuano ya kombe la mabara mwaka 2003, aliwahi kuzichezea West Ham na Manchester City katika miaka ya 2000 na kwenye timu zote mbili alikuwa akipendwa na mashabiki kutokana na jinsi alivyokuwa akicheza kwa moyo na ujasiri mkubwa.
Ishara hiyo itafanywa kwenye dakika ya 23 ya mchezo utakaopigwa kwenye uwanja wa Etihad ambapo mashabiki wa timu zote watasimama na kupiga makofi kwa dakika nzima.
Foe atabaki kwenye historia ya Man City daima baada ya kufunga bao la mwisho kwenye uwanja wa zamani wa City wa Maine Road kabla ya uwanja huo kubomolewa, alifariki dunia baada ya kuanguka uwanjani ambapo madaktari waliomfanyia vipimo waligundua ugonjwa wa moyo ambao ni wa kurithi ndio ulikua chanzo cha kifo chake.




No comments: