PSI

PSI

Thursday, June 28, 2012

BAADA YA HAZARD, NASRI, SNEIJDER NA BENZEMA SASA NI MODRIC - MANCHESTER UNITED WAFELI TENA KWENYE SOKO LA USAJILI

Kama mwanaume ambaye hapendi kukubali kuwa wa pili kwa ubora, Sir Alex Ferguson lazima atakuwa akiudhiwa sana na namna jinsi amekuwa akiwakosa wachezaji anaotaka kuwasajili hasa kwenye miaka ya karibuni kabla ya kugeukia kwa wachezaji wa plan B.

Mchezaji mpya kuongezeka kwenye listi ya ambao Fergie amewataka lakini akawakosa ni Luka Modric, ambaye Sir Alex  amekuwa akimuwania kwa miaka sasa na alitaka kumsaini ndani ya klabu yake ya Manchester United kwa misimu miwili iliyopita.

Katika mara mbili zote, kikwazo kikubwa kimekuwa ni bei ambayo Tottenhma Hotspur wamekuwa wakiitaka £40million kwa Croatia huyo na United kugoma kulipa au kushindwa kumudu bei ambayo inapingana na sera zao za usajili.

Modric angekuwa mtu sahihi kwenye kikosi cha United. Mrithi halisia wa Paul Scholes ambaye anaweza kuimudu nafasi ya kiungo wakati, mchezaji huyo wa zamani wa Dinamo Zagreb sasa kuna uwezekanao mkubwa akajiunga na Real Madrid, huku kuondoka kwake White Hart Lane kukionekana hakuzuiliki.

Hali hii imekuwa ya kawaida kwa United tangu kuwasili kwa kwa wamiliki wapya wa klabu hiyo mwaka 2005. Wakati mabingwa hao wa mara 19 wa soka la England wakiwa na historia kubwa na ubora wa kikosi chao, mikataba ya mamilioni ikiendelea kumiminika na umaarufu ukizidi kukua miongoni mwa mashabiki wa soka duniani.

Ferguson alitumaini jambo hili lingebadilika msimu huu, lakini kuchelewa kwa mipango ya wamiliki wa klabu kuingia kwenye soko la hisa la Singapore kumewafanya United kukosa fedha nyingi za kupambana kwenye soko la usajili.

Ferguson amekuwa akiongea juu ya kukosekana kwa thamani ya ukweli kwenye soko la usajili, lakini mashabiki wa United wanakumbuka wakati Mscotland huyo alivyokuwa akifurahia kuvunja rekodi za usajili wakati alipokuwa akiwanunua akina Jaap Stam, Juan Sebastian Veron na Rio Ferdinand.

Dimitar Berbatov, alisajilia kutoka Spurs kwa ada ya £30.75million mwaka 2008, labda ndio pekee ambaye tunaweza kumtoa kwenye listi kwa kuwemo ndani ya kipindi cha utawala wa Glazers lakini United hawakuwa na upinzani mkubwa kwa ajili saini yake na mahitaji yake binafsi ya mshahara yalifikia sera ya usajili na bajeti ya Manchester United.

Hilo hilo haliwezi kusemwa kwa Eden Hazard, mbelgiji ambaye alikata United na majirani zao City na kusajili Chelsea mwezi uliopita.

United walihisi wapo kwenye nafasi nzuri ya kumsaini Hazard kutoka Lille, lakini hawakuwa radhi kumlipa mchezaji zaidi ya £130,000 kwa wiki achilia mbali fedha ya wakala wake £6million.

Chelsea wakawazidi United kwa kutoa ofa ya £200,000 kwa wiki na kukubali kulipa fedha za wakala, wakawalazimisha United kumgeukia mchezaji aliyekuwa kwenye plan B na wakamsajili Shinji Kagawa kutoka Borussia Dortmund.

Kiangazi kilichopita, United walishindwa tena na mahasimu wao Manchester City katika mbio za kumsaini Samir Nasri kutoka Arsenal kwa kushindwa kutoa ofa ya mkataba wa £170,000 kwa wiki. Wesley Sneijder, target mwingine wa usajili, alikataa kukubali kushusha mahitaji yake ya kupata mshahara wa £200,000 na akabaki Inter Milan.

Mara nyingine zimekuwa sababu za kisoka kwa United kuwakosa wachezaji wanaowataka. Ferguson alikuwa akimuimbisha Karim Benzema kwa takribani miaka miwili lakini mshambuliaji huyo wa kifaransa alikuwa ameweka nia ya kuichezea Real Madrid, wakati David Villa alikuwa hayupo radhi kuondoka Spain na akasaini kuichezea Barelona akitokea Valencia mwaka 2010.

Lakini wachezaji hawa wa hadhi ya juu - miongoni mwa walio bora duniani kwenye nafasi zao ndio ambao United wanahitaji kama ikiwa wanataka kuurudisha ubingwa wa England kwenye kabati la makombe pale Old Trafford na kuweza kutoa ushindani kwenye michuano ya Ulaya.

Ni vipi Ferguson anaweza kuongelea bei kubwa za wachezaji wakati yeye ni mmoja ya watu waliochangia hilo hasa ukizingatia alimuuza Cristiano Ronaldo kwa bei £80million cash kwenda Real Madrid 2009? Hi ni bei ambayo kwa wakati ule angeweza kuinunua klabu nzima ya Newcastle.

Fergie anajua vizuri thamani ya wachezaji wa kisasa kwenye soko la usajili - na anajua kwamba hana fedha za kuwasajili kulingana na bajeti anayopangia na mabosi wake.

United wana deni linalokaribia £500million pamoja na riba yanaizuia klabu hiyo kwenye kushindana kwa fedha na klabu kama City, Chelsea na mabwana wawili wa ligi ya Spain.

Manchester United hawahitaji sugar daddy kama ilivyo kwa Chelsea na City - mapato yao ni hatari, ni fedha nyingi sana - lakini deni kubwa walilonalo wamiliki linaikabaka klabu hiyo shingoni. Na ukweli bila kupata uwekezaji mkubwa kuna hatari City watawapa taabu sana na hata kuwashinda kama klabu inayoongoza England kwenye miaka kadhaa ijayo mbeleni.


No comments: