Barcelona wametangaza kwenye mtandao wao
rasmi kwamba wamekubalina na Valencia juu ya ada ya uhamisho wa
mchezaji wa kimataifa wa Spain Jordi Alba.
Barca ambao wamekuwa
wakihusishwa na beki huyo wa kushoto kwa muda mrefu sasa, wamepiga hatua
kubwa kuelekea kukamilisha dili hilo lenye thamani ya ‹€14 million.
Alba atakwenda Barcelona kufanya vipimo wiki ijayo, na kusaini dili la mkataba wa miaka 5 mara tu atakapofaulu vipimo vya afya.
"Barcelona
wametangaza kwamba makubaliano rasmi yamefikiwa juu ya ada ya uhamisho
wa Jordi Alba, kilichobaki ni vipimo vya afya ambavyo mchezaji huyo
atafanyiwa wiki ijayo jijini Barcelona." Uliandika mtandao huo wa Barca.
"Gharama za uhamisho huu ni €14million na mchezaji atasaini mkataba wa miaka 5."
Alba
mwenye miaka 25 ni zao la chuo cha soka cha Barcelona La Masia, lakini
alifeli kufanikiwa kuingia kwenye kikosi cha kwanza pale Nou Camp na
akaondoka mwaka 2005
|
No comments:
Post a Comment