MOURINHO ATOA AMRI: MASHABIKI CHELSEA WASIMBEZE STEVEN GERRARD
Demba Ba (kushoto) akimfunga Simon Mignolet baada ya Gerrard kuanguka katika uwanja wa Anfield mwishoni mwa msimu uliopita
Jose Mourinho amewaamuru mashabiki wa Chelsea kuacha kuimba nyimbo za kumbeza Steven Gerrard ambaye alisababisha Liverpool ikose ubingwa msimu uliopita.
Mashabiki
wa Chelsea bado hawasahau mwezi aprili mwaka jana ambapo Gerrard
alianguka peke yake na kumruhusu mshambuliaji wa zamani wa Mourinho,
Demba Ba kufunga goli.
Mourinho
ameenda mbali zaidi akisema kipigo cha 2-0 walichopata Liverpool katika
uwanja wa Anfield mwaka jana uliwapa ubingwa Manchester City na kuanzia
siku hiyo mashabiki wa Chelsea wamekuwa wakimbeza Gerrard.
Mashabiki huwa wanaimba: ‘Steve Gerrard, Gerrard, he fell on his f****** a***, he gave it to Demba Ba.’ Hatujaona haja ya kutafsiri kwa sababu za kimaadili.
Picha hii inaonesha kosa alilofanya Gerrard ambalo Jose Mourinho amesema liliwapa ubingwa Manchester City.
Nyimbo za
kumbeza Gerrard zinatarajia kusikika Anfield kesho jumanne wakati
Chelsea inakabiliana na Liverpool kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali
ya kombe la Ligi ‘Capital One’.
Lakini
Mourinho aliyelalamika kuwa Stamford Bridge imekuwa kimya sana,
amesisitiza kuwa mashabiki waache kuimba nyimbo hizo za kumbeza nyota
huyo anayetaka kwenda Marekani.
Amesema:
“Ni mchezaji wa historia wa Liverpool, mchezaji wa kihistoria wa ligi
kuu. Ni mpinzani ambaye mara zote nampenda na kumheshimu. Kuna wimbo
ambao mashabiki wangu wanaimba, siupendi kabisa”.
“Mara zote
wimbo unafurahisha, lakini kuimba, kuimba na kuimba hasa kwa mchezaji
kama yeye, hapana, anastahili heshima, sihitaji dharau”
No comments:
Post a Comment