PSI

PSI

Sunday, June 10, 2012

Beckham ataka unahodha

Beckham alitia saini mkataba mpya na timu ya Marekani ya LA Galaxy mapema wiki hii, na kati ya makubaliano aliyoyafanya ni klabu kumruhusu kushiriki katika mashindano ya London.
"Ningelipenda sana kuwa nahodha", mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 alielezea. "Nimewahi kuiongoza nchi yangu, na ninaelewa hili ni jambo muhimu sana katika kuiongoza timu katika Olimpiki."
"Nimezungumza na Stuart Pearce (kocha), lakini bado sijachaguliwa."
Beckham alikuwa ni kati ya watu waliokuwemo katika kundi la kuongoza kampeni za London za kuandaa mashindano waliofika Singapore mwaka 2005.

No comments: