Mabingwa wa Dunia Uhispania imeanza utetezi wa Kombe
lao la ubingwa wa mashindano ya Ulaya kwa sare ya 1-1 dhidi ya Italia
katika pambano la kundi C mjini Gdansk.
Italia ndiyo iliyotangulia baada ya kipindi cha
kwanza kumalizika bila bao lolote kufungwa na alikua Antonio Di Natale
aliyeingia badala ya Balloteli kufunga bao katika dakika ya 60.Dakika nne baadaye Mabingwa wa Dunia na Ulaya walifumania lango la Italia na licha ya juhudi na umahiri wa Mabeki David Silva alimuona Cesc Fabregas na kumuwekea pasi maridhawa na bila kufanya makosa akaupenyeza mpira kumpita goli wa Italia Buffon.
Italia yachacha na Uhispania

No comments:
Post a Comment