AZAM FC imefanikiwa kupata mrithi wa kiungo wao waliyemtimua, George
Odhiambo ‘Blackberry’, baada ya kumnasa mshambuliaji kutoka DR Congo
aliyefahamika kwa jina la Papii.
Odhiambo alitimuliwa wiki
iliyopita kutokana na utovu wa nidhamu uliotokana na kutohudhuria
mazoezi kwa muda wa siku nne mfululizo.
Kwa mujibu wa kiongozi
mmoja kutoka katika benchi la ufundi la timu hiyo ambaye hakutaka
kutajwa jina lake kwa kuwa si msemaji wa timu, alisema mchezaji huyo
aliyemfahamu kwa jina moja la Papii, alianza mazoezi tangu wiki
iliyopita.
Amesema kuwa amekuwa akionyesha uwezo mkubwa mazoezini
hasa katika kupachika mabao. “Kuna mchezaji mpya kaja na ana wiki sasa
anafanya mazoezi, namfahamu kwa jina moja tu la Papii na ametoka Congo,
hucheza nafasi ya ushambuliaji |
No comments:
Post a Comment