PSI

PSI

Monday, August 20, 2012

Simba yashikilia rekodi ya makombe mapya

Simba ilianza kuweka rekodi hiyo ilipotwaa Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara, ilipoanzishwa mwaka 1967, wakati huo klabu hiyo ilikuwa ikijulikana kama Sunderland.
Wekundu hao wakaendelea kwa kunyakua Kombe la Kagame, mara baada ya michuano hiyo kuanzishwa mwaka 1974 na kufanya hivyo tena katika lile la Tusker lililoanza 2002, kombe ambalo walilinyakua mara tatu mfululizo tangu lianzishwe.
Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Bara, mwaka huu waliendeleza ubabe huo katika michuano mingine mipya ya Amani, walipoifunga Azam kwa mikwaju ya penalti katika fainali iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar, kabla ya kufanya hivyo kwenye michuano ya Super 8, juzi, ikiwa imeanzishwa kwa mara ya kwanza

No comments: