PSI

PSI

Monday, September 3, 2012

Van Persie aikoa Man.United

Robin van Persie amegeuka kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu yake mpya kwa kuiokoa Man.United alipofunga matatu mwenyewe kumuondolea maradhi ya moyo Sir Alex Ferguson kunako mechi yake ya 1,000th akiiongoza Manchester United kama meneja.
Mdachi huyo alitanguliza la kichwa kutokana na kona iliyochongwa na Nani katika mda wa ziada kuokoa jahazi.
Southampton ilipata bao la kuongoza kupitia Rickie Lambert kabla ya Morgan Schneiderlin kupata la pili pia la kichwa katikati ya magoli ya Van Persie ya kusawazisha.
Uhodari wa Van Persie uliwekwa kwenya mizani alipokosa mkwaju wa peneti mnamo dakika 88 wakati United ikidorora 2-1.
Kwa menejawa Southampton Nigel Adkins dakika za majeruhi zilikua kama mwaka wenye machungu kutokana na jinsi vijana wake walivyoweza kuidhibiti United na mabao ya haraka haraka mawili bila shaka yalimuumiza.
Kwa mashabiki wa United, matokeo haya ni sehemu ya malipo ya kitita cha milioni 24 za pauni za Uingereza zilizomleta United kutoka Arsenal.

No comments: