Robin van Persie amegeuka kuwa kipenzi cha mashabiki
wa klabu yake mpya kwa kuiokoa Man.United alipofunga matatu mwenyewe
kumuondolea maradhi ya moyo Sir Alex Ferguson kunako mechi yake ya
1,000th akiiongoza Manchester United kama meneja.
Mdachi huyo alitanguliza la kichwa kutokana na kona iliyochongwa na Nani katika mda wa ziada kuokoa jahazi.
Southampton
ilipata bao la kuongoza kupitia Rickie Lambert kabla ya Morgan
Schneiderlin kupata la pili pia la kichwa katikati ya magoli ya Van
Persie ya kusawazisha.
Uhodari wa Van Persie uliwekwa kwenya mizani alipokosa mkwaju wa peneti mnamo dakika 88 wakati United ikidorora 2-1.
Kwa menejawa Southampton Nigel Adkins dakika za
majeruhi zilikua kama mwaka wenye machungu kutokana na jinsi vijana wake
walivyoweza kuidhibiti United na mabao ya haraka haraka mawili bila
shaka yalimuumiza.
Kwa mashabiki wa United, matokeo haya ni sehemu
ya malipo ya kitita cha milioni 24 za pauni za Uingereza zilizomleta
United kutoka Arsenal. |
No comments:
Post a Comment