PSI

PSI

Saturday, August 3, 2013

Bale awaaga wachezaji wenzie Spurs .

Kiungo mshambuliaji wa Tottenham Hotspurs Gareth Bale hapo jana aliwaaga rasmi wachezaji wenzie ikiwa ni ishara ya kukaribia kwake kuihama klabu hiyo kujiunga na Real Madrid .
Bale aliwaaga wachezaji wa Spurs kwa kutia saini za kumbukumbu kwenye jezi zao walipokuwa wanapanda ndege kuelekea nchini Ufaransa ambako watacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Monaco .
Gareth-Bale-1859031
Bale alibaki nyuma jijini London ambako anamalizia sehemu za mwisho za mazungumzo ya uhamisho wake kwenda klabu ya Real Madrid ambayo imekuwa ikimfanya juhudi za kumsajili .
Gareth Bale anatarajiwa kukamilisha usajili huo ndani ya siku chache zijazo na inaaminika kuwa Madrid watalipa ada ya uhamisho ambayo itavunja rekodi ya usajili .

No comments: