PSI

PSI

Saturday, August 31, 2013

Bayern Munich yaifunga Chelsea kwenye UEFA Super Cup.


Kocha Mhispania Pep Guardiola ameiongoza Bayern Munich kutwaa taji lake la kwanza kwa msimu huu baada ya kuifunga Chelsea kwa mikwaju ya penati na kutwaa ubingwa wa UEFA Super Cup.
Chelsea ndio walioanza kupata bao mapema kwenye dakika ya nane mfungaji akiwa Fernando Torres ambaye alifunga kwa shuti akipokea krossi ya Mjerumani Andre Schurrle.
Bayern Munich walisawazisha bao hilo kitia kwa Frank Ribery ambaye alikosa nafasi nyingi za wazi kabla ya kufunga bao hilo mwanzoni mwa kipindi cha Pili.
Mchezo huo uliliazimikankwenda kwenye muda wa nyongeza baada ya dakika tisini kumalizika huku timu zote zikiwa zimefungana bao 1-1 .
Chelsea walipata bao mwanzoni mwa kipindi cha kwanza cha muda wa nyongeza mfungaji akiwa Edin Hazard ambaye alipiga shuti lililomzidi kipa wa Bayern Manuel Neur.
Bayern Munich hawakukata tamaa na waliendlea kushambulia na mashambulizi hayo yalizaa matunda mwishoni mwa dakika za nyongeza wakati kiungo Javi Martinez alipofunga bao la kusawazisha .
Mshambuliaji Romelu Lukaku alishuhudia penati yake ikiokolewa na kipa wa Bayern Neur na kuipa timu hiyo ya Ujerumani ushindi wa penati 5-4.






No comments: