PSI

PSI

Friday, August 30, 2013

Defar, Bolt na Sum watawala Zurich

Meseret Defar wa Ethiopia amedhihirisha umaarufu wake katika mbio za kina dada za mita elfu tano pale alipomshinda Muethiopia mwenzake Tirunesh Dibaba wakati wa mashindano ya IAAF Diamond league zilizofanyika mjini Zurich.
Meseret Defar alizitimuka mbio hizo kwa muda wa dakika 14:32.83, akifuatwa na Dibaba na Mkenya Mercy Cherono, ambaye ni mshindi wa medali ya fedha katika mashindano ya dunia.
Katika mbio za mita elfu moja mia tano kwa wanaume, bingwa wa dunia Asbel Kiprop, alimaliza katika nafasi ya sita, huku mkenya mwezake Silas Kiplagat akiibuka na ushindi.
Ayanleh Souleiman wa Djiobouti akiridhika na nafasi ya pili akifuatwa na Nixon Chepseba.
Bingwa wa dunia wa mbio za mita mia nane kwa kina dada, Euinice Sum kwa mara nyingine tena aliwapiku wapinzani wake katika mbio na kudhihirisha umaarufu wake katika mbio hizo.
Sum alitumia muda wa dakika moja sekunde 58 nukta 82 naye bingwa wa zamani wa dunia Mariya Savinova wa Urussi akimaliza katika nafasi ya pili akifuatwa na Malika Akkoui.

No comments: