PSI

PSI

Saturday, August 3, 2013

Fabregas anaweza kuondoka.


Kocha mpya wa klabu ya Barcelona Gerardo Tata Martino ametoa tamko juu ya mustakabali wa kiungo wa klabu hiyo Cesc Fabregas .
Tata amesema  kuwa uamuzi wa kubaki ama kuihama klabu ya Barcelona upo mikononi mwa mchezaji mwenyewe na hawezi kumuingilia katika uamuzi wowote atakaoufanya .
Kocha huyo ameongeza kuwa anaamini kuwa Cesc anaipenda Barca na hataondoka kwenye klabu hiyo baada ya kuwepo kwa ofa za kumsajili toka klabu ya Manchester United.
Cesc alikuwa uwanjani hapo jana wakati Barca ilipocheza na Santos katika mchezo wa kirafiki ambapo mabingwa hao wa zamani wa ulaya walishinda kwa mabao nane bila huku Cesc akifunga mabao mawili .
Manchester United walipeleka ofa mbili kwa ajili ya kiungo huyu ambapo ya kwanza ilikuwa paundi milioni 26  kabla ya kuja na ya pili ambayo iliongezeka na kufikia paundi milioni 31 . United huenda wakarudi na ofa ya tatu ambayo itakuwa ya mwisho ambayo inaaminika kuwa itafikia paundi milioni 41.


No comments: