Timu zote Jumatatu ziliweza kuonyesha mbinu
nzuri na kila upande kwa muda kuweza kumiliki mpira kwa muda katika
uwanja wa Donetsk, huku jua kali likiangaza, na Joleon Lescott akipata
bao la kwanza la England, kabla Samir Nasri kusawazisha.
"Hii ni nafasi nzuri kwetu kuweza kuimarisha mchezo wetu,” alisema Hodgson baada ya mechi yao ya kwanza, katika kundi D.
"Ni matumaini yetu kwamba tutakuwa bora zaidi.
Kadri tunavyofanya mazoezi na kucheza mechi nyingi, ndivyo
tunavyoimarisha mchezo wetu zaidi.”
Hii ilikuwa ni mechi ya tatu kwa Hodgson tangu achukue hatamu za kuiongoza timu ya taifa ya soka ya England.
Alielezea kwamba aliridhika na mchezo huo, baada
ya kutoka sare na timu ya Ufaransa, ambayo haijashindwa katika kipindi
cha miaka miwili.
Katika mechi ya pili siku ya Jumatatu, Ukraine iliweza kuishinda Sweden magoli 2-1
|
No comments:
Post a Comment