Ashley Cole ameshtakiwa na chama cha kandanda cha
England cha FA, kutokana na ukosefu wa nidhamu, kufuatia na maneno
aliyoyaandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter, kuhusiana na
usimamizi wa chama hicho.
Akiandika baada ya uamuzi wa chama hicho cha
soka kumuadhibu John Terry katika kesi juu yake ya ubaguzi wa rangi,
Ijumaa iliyopita aliandika: "Hahahahaa, vyema kabisa...FA,
nilidanganya?...kundi la ....***".
Mchezaji huyo, ambaye ni mlinzi wa klabu ya
Chelsea, na mwenye umri wa miaka, 31 alikuwa Jumatatu ajiunge na timu ya
taifa ya England.
Cole ana nafasi ya kujitetea juu ya kosa hilo la kukosa nidhamu, kabla ya saa kumi, Alhamisi, tarehe 11 Oktoba.
Cole
aliandika maneno hayo kufuatia uamuzi wa tume huru ya FA, ambayo
ilimpata John Terry na hatia ya kutumia matamshi ya ubaguzi wa rangi
dhidi ya Anton Ferdinand wakati wa mechi kati ya Chelsea na QPR msimu
uliopita.
Baadaye Cole alikiomba radhi chama cha FA.
Mbali
na kufuta maneno aliyoyaandika, aliandika taarifa ikielezea: "Nilikuwa
nimemaliza mazoezi tu nilipoyaona yale yaliyotangazwa katika televisheni
kuhusiana na niliyoyasema juu ya chama cha FA.
"Yalinisikitisha
mno, kwani nilikuwa nimeandika hisia zangu kwa haraka katika joto la
matukio hayo. Ninakiomba radhi mno chama cha FA kwa maneno yangu."
Nahodha
wa zamani wa timu ya taifa ya England, Alan Shearer, mwishoni mwa wiki
alisema inafaa Cole apigwe marufuku asicheze mechi ya Ijumaa ya kufuzu
kwa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, dhidi ya San Marino.
|
No comments:
Post a Comment